Monday, September 12, 2011

Simba na Azam zaingiza Ml. 72


Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa Septemba 11 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 72,167,000.

Kwa mujibu wa msemaji wa Shirikisho hili Boniface Wambura, Watazamaji waliokata tiketi kwa ajili ya kushuhudia mechi hiyo walikuwa 21,129. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 15,000, sh. 7,000, sh. 5,000 na sh. 3,000.

Viti vya bluu na kijani ambavyo kiingilio kilikuwa sh. 3,000 viliingiza watazamaji 18,586, hivyo kuingiza sh. 55,758,000.

No comments:

Post a Comment