Thursday, September 8, 2011

Maria Mutola ajiunga na Soka

Maria Mutola


Wakati Maria Mutola alipomaliza fainali za mbio mita 800 kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Beijing, huku akiwa na umri wa miaka 35, ilionekana kwamba huo ndio ungekuwa mwisho wa mwana mama huyo aliyepachikwa jina la "Maputo Express" kwenye dunia ya kimichezo.

Ila baada ya miaka mitatu, akiwa amestaafu kwenye mbio, Mutola ameamua kujikita kwenye mpira wa miguu, na safari hii akiwa nahodha wa timu ya Msumbiji

Mutola, anaiwakilisha nchi hiyo kwenye mashindano ya All-Africa Games yanayoendelea nchini kwao kwenye jiji la Maputo. 

Mertesacker ajifananisha na Tonny Adams

Per Mertesacker

Beki mpya wa Arsenal Mjerumani Per Mertesacker, anaamini ataweza kufata nyayo za beki wazamani wa timu hiyo Tony Adams, hii ni katika kuelekea kwenye mechi yake ya kwanza akiwa na washika bunduki wa Emirate siku ya Jumamosi dhidi ya Swansea.

Mertesacker anatakiwa aendane na mfumo wa vijana wa Wenger haraka, beki wa timu hiyo Thomas Vermaelen yuko atakuwa nje ya dimba kwa wiki sita, baada a kufanyiwa upasuaji wa enka siku ya Jumatatu.
Mjerumani huyo, ambaye amejiunga na Klabu hiyo akitokea Werder Bremen kwa gharama ya £8 ml, anataka kuwa sehemu ya wachezaji watakao rudisha mafanikio ya timu ya Arsenal.
Tonny Adam alikuwa nahodha wa timu hiyo kwenye moja kati ya vipindi vya mafanikio ya Klabu hiyo, Mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal aliiwezesha timu hiyo kushinda vikombe Vinne vya Ligi, huku wakati flani akiweza kubeba kombe hilo mara mbili mfululizo chini ya Wenger.
"Hatukuwa na taswira yake kwenye Tv, ila Adam aliheshimika sana hapa, yeye ni mtu muhimu kwangu," Mertesacker aliueleza mtandao wa Klabu ya hiyo. 

"Nilipokuwa naangalia Ligi ya Uingereza, mara nyingi nilikuwa nawaatazama Arsenal, hakika alikuwa ni beki mzuri sana, kipindi hicho nikiwa na miaka 10 au 12 hivi, nawapenda wachezaji kama  Adams sana tu – Nimekuwa nikifurahi kuwangalia kwa miaka mingi.
" Natumai nitaongeza kiwango changu hapa na kuwa bora na bora – nataka niwe mtu muhimu kwenye timu."

Ronaldo: Nataka kushinda CL na Madrid

Cristiano Ronaldo

Mshambuliaji wa timu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo, amesema shabaha yake kuu msimu huu ni kushinda Champions League.
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, anaamini kushinda Kombe hilo la Ulaya ndio yatakuwa mafanikio makubwa pale Santiago Bernabeu kwa msimu huu.
"Inatubidi tushinde Makombe muhimu, La Liga au Champions League sababu, haya ndiyo makombe yanayokufanya uone kama umeshinda kitu kwenye mpira," aliueleza mtandao wa Uefa.
"Kushinda Champions League ni hatua ya mwisho kuhesabu kwamba umemaliza msimu sababu ni moja kati ya makombe muhimu.
Madrid watakutana na Dinamo Zagreb wiki ijayo kwenye Champions League, ikiwa ni mchezo wa kwanza wa Kundi D, kabla ya hapo wataanza kuwakaribisha Getafe kwenye uwanja wa nyumbani Santiago Bernabeu, katika mechi ya La Liga siku ya Saturday.

Usishangae Beckham QPL January

David Beckham

Litakapokuja kufunguliwa dirisha la usajili, usishangae Queens Park Rangers wakionyesha nia ya kumtaka David Beckham, ambaye mkataba wake kwenye Major League Soccer unaisha mwezi November.
"Ila hiyo haitakuwa mpaka mwezi January, hakika hiki si kitu cha kuzungumza kwa sasa." Haya ni maneno ya Kocha mkuu wa timu hiyo Neil Warnock.
"Hatuwezi kumsajili ila, hatuwezi kumsajili mtu yoyote kwa sasa mpaka January, kwa nini muwe na wasi?" Warnock alisema siku ya Alhamisi, wiki moja baada ya dirisha la usajili kufungwa.
"Nadhani ni mchezaji wa kipekee, na amekuwa hazina kubwa kwa soka la Uingereza, nampenda kama mtu ila niulize itapofika January.” Alisema Warnock.

Guardiola apewa tunzo na Bunge la Catalonia

Pep Guardiola

Kocha wa Klabu ya Barcelona Pep Guardiola, amepewa Tunzo ya Dhahabu ya mafanikio na Bunge la Catalonia.

Tunzo hiyo inatambua mchango wake toka alipoichukua timu hiyo kipindi cha majira ya joto ya mwaka 2008, baada ya kuwa kocha wa timu B ya Barcelona kwa mwaka mmoja.

"Nilichaguliwa kuwa Kocha wa Barca na faida ilikuwa ni kwa wale walionichagua, huku hii ikiwa njia nzuri ya kukabiliana na kazi yangu," alisema.

Guardiola ameiongoza na kuipa Barca jumla ya makombe 12, mawili ya Kombe la Mabingwa Ulaya, na matatu yakiwa ni mataji ya La Liga.

Balotelli ahusishwa na Kundi la Kijasusi la Mafia

Mario Balotelli
Mikasa inayomkumba Mario Balotelli toka ajiunge na Klabu ya Manchester City imechukua hatua nyingine, safari hii mchezaji anatakiwa na Jeshi la Polisi la nchini Italia kuelezea mahusiano yake na Kundi la Kijasusi la Mafia.

Balotelli, ambaye amejiunga na Klabu hiyo kwa wa £24 ml toka Inter Milan mnamo mwaka jana, ameitwa kama shahidi na waendesha mashtaka wa jiji la Naples, lengo likiwa ni kuweza kusaidia uchunguzi unaoikabili kundi la Mafia.
Inasemekana mchezaji huyo, alionekana akiwa sambamba kwenye msafara wa moja kati ya makundi ya kiharifu yaliyopo jijini Naples, makundi yanayoongozwa na Mario Iorio, mmoja kati ya watu wanaojishughulisha na biashara ya kusambaza vyakula.
Huku ikielezwa, Lorio anahusishwa na kashfa ya utengenezaji noti bandia, kesi yake ikiwa inaendelea.

"Hakuna kitu cha kuogopa, niko poa, sikuwa na wazo na watu waliokuwa wanapita karibu yangu ni kina nani," Balotelli alisema alipoulizwa kuhusiana na ishu hiyo.
"Siku ile kulikuwa na watu wengi karibu yangu, najisikia vibaya sababu inaweza kuithiri familia yangu, nilichokuwa nataka nione pale ni namna gani lile eneo linafanana na vile ambavyo huwa naliona kwenye filamu ya Gomorrah."

Rooney amuhitaji Chicharito haraka

Rooney & Hernandez

Wayne Rooney amesema, angependa kuungana na mchezaji mwenzake Javier Hernandez kwenye safu ya ushambulizi ya timu hiyo mapema zaidi.

Wachezaji hao wawili, msimu uliopita wa EPL walitengeneza safu kali ya ushambuliaji, safu iliyosaidia kuipa Manchester United ubingwa wake wa 19 wa Ligi hiyo.

"Naamini tulichokifanya na Hernandez msimu uliopita tutakifanya pia msimu huu, tutafunga magoli mengi," Rooney aliieleza MUTV.

"Hakika watu wanamfahamu kwa sasa ila, kama ukiangalia wachezaji wakali Duniani, huwa wanafahamu wanacheza na nani na ni ngumu kuwazuia.

"Mienendo yake ndani ya uwanja ni mizuri, na ni ngumu kuizuia. Si rahisi kwa wachezaji kumzuia, wawe wanamfahamua ama kinyume chake.

"Ni vizuri kuwa na mwenza ambaye amefika kwenye timu, ambaye anaweza kuongea Kingereza kizuri na kila wakati ana tabasamu." Alisema Rooney.

Ayew kukosa mechi ya ufunguzi CL

Andre Ayew

Mchezaji nyota wa Timu ya Taifa ya Ghana Andre Ayew, atakosa mechi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya, wakati timu yake ya Marseille itakapokuwa inacheza na Olympiakos siku ya Jumanne.

Ayew 21, anasumbuliwa na maumivu ya kifundo, yatamsababisha pia asiwepo kwenye mechi ya kwanza ya Ligue 1, ambayo Timu yake itacheza dhidi ya Stade Rennes wekiendi hii.

"Andre Ayew anategemea kuwa nje ya uwanja kwa siku 10, baada ya kuumia kwenye mechi aliyokuwa anaitumikia Ghana," FA ya Ghana imeeleza kwenye mtandao wake leo.

"Mchezaji huyo wa Marseille alipata jeraha hilo wakati Ghana ilipokuwa inacheza na Swaziland, kwenye mechi ya kusaka nafasi ya kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika Ijumaa iliyopita." Taarifa hiyo ilisema.

Twiga Stars yatoka sare na Banyana


Timu ya Taifa ya wanawake ya Tanzania (Twiga Stars) imetoka sare ya mabao 2-2 na Afrika Kusini (Banyana Banyana) katika mechi ya michezo ya All Africa Games (AAG) iliyochezwa leo Uwanja wa Machava jijini Maputo, Msumbiji.

Banyana Banyana ndiyo iliyoanza kupata bao kabla ya Twiga Stars kusawazisha dakika ya 25 kupitia kwa Mwanahamisi Shuruwa.

Banyana Banyana ilianza kipindi cha pili kwa nguvu na kupata bao la pili. Zena Khamis aliisawazishia Twiga Stars dakika 60.

Twiga Stars itacheza mechi yake ya mwisho hatua ya makundi Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe kwenye uwanja huo huo. Katika mechi yake ya kwanza Zimbabwe ilifungwa na Banyana Banyana mabao 4-1.

Tarehe ya Rufaa ya Bin Hammam yatajwa

Mohamed Bin Hammam

Shauri la aliyekuwa mgombea nafasi ya Urais wa FIFA Mohamed Bin Hammam, juu ya kupinga adhabu ya kifungo cha maisha aliyopewa kutojihusisha na masuala ya mpira, limepangwa kusikilizwa wiki ijayo.

FIFA wamethibitisha.

Kamati ya rufaa ya FIFA, inategemea kusikiliza shauri hilo siku ya Alhamisi, September 15, ambapo Bin Hammam anapinga adhabu hiyo, iliyotolewa na kamati ya maadili ya Shirikisho hilo mnamo mwezi July.

Shauri hilo linaweza kamilika siku hiyo japo kuna uwezekano linaweza kwenda mpaka September 16.

Simba na Yanga ruhsa kutumia Uwanja wa Taifa

Uwanja wa Taifa

Serikali imeruhusu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutumika kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zinazohusu timu za Simba na Yanga. Hata hivyo ruhusa hiyo ni ya mechi mbili kwa wiki.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na klabu za VPL zenye maskani yake Dar es Salaam waliwasilisha tena maombi Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ili kutumia uwanja huo kwa mechi za ligi.

Kutokana na uamuzi huo wa Serikali mechi ambazo sasa zitachezwa kwenye uwanja huo ni Ruvu Shooting vs Yanga (Septemba 10), Azam vs Simba (Septemba 11), Simba vs Polisi Dodoma (Septemba 14), African Lyon v Yanga (Septemba 15), Azam vs Yanga (Septemba 18), Yanga vs Villa Squad (Septemba 21).

Nyingine ni Yanga vs Coastal Union (Septemba 24), Simba vs Mtibwa Sugar (Septemba 25), Yanga vs Kagera Sugar (Oktoba 14), Simba vs African Lyon (Oktoba 16), Simba vs Ruvu Shooting (Oktoba 19), Yanga vs Toto Africans (Oktoba 20), Simba vs JKT Ruvu (Oktoba 22), Yanga vs Oljoro (Oktoba 23), Yanga vs Simba (Oktoba 29) na Moro United vs Simba (Novemba 5).

Nafasi ya Torres Hispania shakani

Fernando Torres

Fernando Torres ameelezwa na Kocha wa Timu ya Taifa lake Vicente del Bosque kwamba, anaweza kupoteza nafasi yake kwenye kikosi hicho, kama atashindwa kufunga magoli mara kwa mara kwenye timu yake ya Chelsea .

Nafasi yake kwenye timu ya Chelsea inatishiwa na uwepo wa wachezaji kama Didier Drogba, Nicolas Anelka na Romelu Lukaku, kitu ambacho kinatisha nafasi yake pia kwenye timu ya taifa. lake.

Del Bosque hakumpa nafasi Torres hata yakuwepo kwenye benchi, kwenye mechi ambayo Hispania ilishinda kwa magoli 6-0 dhidi ya Liechtenstein, kitendo kilichomfanya mshambuliaji huyo kuangalia mechi hiyo akiwa jukwaaini.

"Torres ni mchezaji muhimu, ila wale wanaofanya vizuri kwenye klabu zao ndio wataoitwa timu ya Taifa, na si kinyume na hapo," alisema Del Bosque.

Torres hajaifungia timu yake ya taifa toka alipofunga kwenye mechi dhidi ya Liechtenstein miezi 12 iliyopita.

Dalglish amtetea Carroll

Andy Carroll

Meneja wa Klabu ya Liverpool Kenny Dalglish, amemtetea mchezaji wake Andy Carroll, kufuatia shutuma alizotupiwa na Kocha wa Timu ya Taifa ya Uingereza Fabio Capello, juu ya kiwango cha mchezaji huyo na tabia ya anasa inayoporomosha kiwango chake.

Mapema wiki hii, Mtalianao huyo alisema: "Andy anahitaji kuwa makini. Sijui chochote kuhusu aina hii ya maisha, ni matatizo binafsi ambayo siwezi kuyazungumzia.

"Ila kama anahitaji kuwa mchezaji mzuri na mwanamichezo, anahitaji apunguze kupunguza kunywa, hayupo kwenye kiwango chake cha juu kwa sasa."

Ila Dalglish ambaye alitumia kiasi cha £35m mwezi January alimtetea kwa kusema, "kwetu sisi tumezungumza mara kadhaa, ila imeangukia kwenye sikio la kiziwi, Andy hakuwa fiti kiasi cha kutosha msimu uliopita sababu ya majeraha,'' alisema meneja huyo.

"Tumeridhishwa na kiwango cha ufiti wake kwa mwaka huu, sababu ameondokana na majeraha yaliyokuwa yanamkabili."

"Haufahamu maisha yake, nani anafahamu maisha yake? Andy, nadhani ni mtu mwenye hekima zaidi ya watu wengi sana, na sidhani mwenendo wa maisha wake si kitu pale wanapotaka kuandika habari zao.

"Nadhani anashukuru ushauri wa Fabio Capello, na anamuheshimu sana Fabio Capello - na naamini pia Fabio Capello anamuheshimu sana Andy Carroll.''

Mancini aeleza sababu ya kumsajili Hargreaves

Roberto Mancini

Meneja wa Timu ya Manchester City Roberto Mancini, amesema mwanzoni nia yake kuu ilikuwa ni kumsajili mchezaji wa Roma Daniele de Rossi au mchezaji wa  Real Madrid Fernando Gago - ila akasema sababu za kifedha ndizo zilizosababisha amsajili Owen Hargreaves.

Mancini aliieleza the Independent: "Gago ndiye mchezaji tuliyemtaka kwa udi na uvumba, hatukutaka tutumie hela zaidi ya ile tuliyoipanga.

"De Rossi ni mmoja kati ya viungo wazuri hapa Duniani, ila siamini kama anaweza kuondoka Roma. Kwa hiyo kwenye kiungo tukaamua kumsajili  Hargreaves, ambaye yuko nje ya mkataba.''

Chelsea: Hatumuhitaji Modric tena

Andre Villas-Boas

Kocha wa Timu ya Chelsea Mreno Andre Villas-Boas, amesema baada ya kumsajili aliyekuwa kiungo wa timu ya Liverpool Raul Meireles, hatomuhitaji tena mchezaji aliyekuwa anamtaka kwa kipindi kirefu, kiungo mchezeshaji wa timu ya Tottenham Hotspur Luka Modric.

Alipoulizwa kama Chelsea watarudi na kumsajili tena mchezaji huyo wa Tottenham katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo mwezi January, Villas-Boas alisema: "Hapana, sidhani. Soko limeshafungwa na siwezi bashiri kitakachotokea mwezi January."

Vile vile kocha huyo, Villas-Boas amesikitishwa kwa kushindwa kumsajili beki wa kushoto toka Uruguay Alvaro Pereira, ambaye anakipiga na Klabu ya Porto.

"Tulikuwa mbali kuweza kufikia kiwango cha matakwa ya Porto kwa mchezaji huyo. Niko na furaha nikiwa na Ashley Cole na Ryan Bertrand."

Wakati huo huo, Didier Drogba, anakimbizana na muda kuweza kuwa fiti ili aweze kuwemo kwenye mechi ambayo Chelsea watacheza na Manchester United.

Kocha wa Blues Andre Villas-Boas amesema, mshambuliaji huyo atakosa mechi ya Jumamosi hii dhidi ya Sunderland, na ile ya Jumanne ya Kombe la Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Bayer Leverkusen.