Thursday, September 8, 2011

Maria Mutola ajiunga na Soka

Maria Mutola


Wakati Maria Mutola alipomaliza fainali za mbio mita 800 kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Beijing, huku akiwa na umri wa miaka 35, ilionekana kwamba huo ndio ungekuwa mwisho wa mwana mama huyo aliyepachikwa jina la "Maputo Express" kwenye dunia ya kimichezo.

Ila baada ya miaka mitatu, akiwa amestaafu kwenye mbio, Mutola ameamua kujikita kwenye mpira wa miguu, na safari hii akiwa nahodha wa timu ya Msumbiji

Mutola, anaiwakilisha nchi hiyo kwenye mashindano ya All-Africa Games yanayoendelea nchini kwao kwenye jiji la Maputo. 

No comments:

Post a Comment