Thursday, September 8, 2011

Ronaldo: Nataka kushinda CL na Madrid

Cristiano Ronaldo

Mshambuliaji wa timu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo, amesema shabaha yake kuu msimu huu ni kushinda Champions League.
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, anaamini kushinda Kombe hilo la Ulaya ndio yatakuwa mafanikio makubwa pale Santiago Bernabeu kwa msimu huu.
"Inatubidi tushinde Makombe muhimu, La Liga au Champions League sababu, haya ndiyo makombe yanayokufanya uone kama umeshinda kitu kwenye mpira," aliueleza mtandao wa Uefa.
"Kushinda Champions League ni hatua ya mwisho kuhesabu kwamba umemaliza msimu sababu ni moja kati ya makombe muhimu.
Madrid watakutana na Dinamo Zagreb wiki ijayo kwenye Champions League, ikiwa ni mchezo wa kwanza wa Kundi D, kabla ya hapo wataanza kuwakaribisha Getafe kwenye uwanja wa nyumbani Santiago Bernabeu, katika mechi ya La Liga siku ya Saturday.

No comments:

Post a Comment