Saturday, September 10, 2011

Mrithi wa Genevive kupatikana leo

Genevive Miss Tanzania 2010
SHINDANO la kumsaka mrembo wa Miss Tanzania linafanyika leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Jumla ya warembo 30 watapanda jukwaani kuchuana vikali kuwania zawadi ya gari aina ya Jeep Patriot yenye thamani ya shilingi 72 milioni.
Warembo hao wataonyesha vazi la ubunifu, ufukweni na vazi la usiku.
Mshindi atapata fursa ya kuiwakilisha Tanzania kwenye shindano la urembo la dunia 'Miss World' litakalofanyika baadaye mwaka huu.

Yanga kukata kiu ya mashabiki wake leo?

Mashabiki wa Yanga
MASHABIKI wa Yanga wenye kiu ya ushindi wa takribani siku 62, watajazana kwenye Uwanja Taifa kuwaongoza mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu kusaka pointi tatu dhidi ya vibonde Ruvu Shooting leo.

Yanga wanashuka uwanjani hapo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba katika mechi ya fainali ya Kombe la Kagame iliyofanyika Julai 10 yakiwa ni matokeo yao mazuri ya mwisho katika mechi zaidi ya saba walizocheza tangu wacheze mechi hiyo.

Mabingwa hao walikuwa kwenye wakati mgumu kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro waliouteua kuwa uwanja wa nyumbani baada ya serikali kuufunga Uwanja wa Taifa kwa takribani wiki mbili.

Katika mchezo wa leo dhidi ya Shooting, vijana hao wa mtaa wa Twiga na Jangwani wanajua mashabiki wao wana hamu kubwa ya kuona timu hiyo ikirudisha heshima yake kwa kushinda mchezo wa kwanza katika Ligi Kuu.

Picha Bora ya Wiki ya Kimichezo

Luis Suarez

Maradona: Sijawahi angalia mechi ya Argentina

Diego Maradona

Kocha wa timu ya Al-Wasl Diego Maradona, amesema hawezi thubutu kuangalia mechi ya Timu ya Taifa ya Argentina.
Kocha huyo ambaye hivi karibuni ameanza kutafuta mafanikio mapya Mashariki ya Kati amesema, " Toka nilipoondoka, sijawahi kuangalia hata mechi moja ya Argentina"
"Sidhani kama ntakuja kuangalia tena, najua itaniumiza" alisema nguli huyo wa zamani mwenye miaka 50 sasa.

"Sina deni na mtu, nilijitahidi kujitoa kwa yote kwa wachezaji, nao walifanya kwangu kama mimi ilivyofanya kwao."

"Hatukuweza kuwapa Wa-Argentina kile walichopaswa kukipata, ambacho kilikuwa ni Kombe la Dunia, ila tulijitahidi kadiri tulivyoweza, na tunajiangalia kwenye kioo na fahari."
Zlatan Ibrahimovic

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Italia maarufu kama Seria A AC Milan, wameshindwa kuanza vyema kutetea taji hilo, baada ya kwenda sare ya 2-2 na Lazio, kwenye uwanja wao wa San Siro jana Ijumaa.
Wageni ndio waliokuwa wa kwanza kuingiza nyavuni bao zote mbili, kwa magoli yaliyofungwa na washambuliaji wapya Miroslav Klose na Djibril Cisse.
Zlatan Ibrahimovic na Antonio Cassano waliweza kuipatia Inter magoli ya kusawazisha na kuifanya mechi iishe kwa sare.

Mechi za EPL leo Jumamosi

Jumamosi, 10 September 2011
Muda ni kwa Saa za Bongo


Arsenal v Swansea, 17:00
Everton v Aston Villa, 17:00
Man City v Wigan, 17:00
Stoke v Liverpool, 17:00
Sunderland v Chelsea, 17:00
Wolverhampton v Tottenham, 17:00
Bolton v Man Utd, 19:30

Tevez anyang'anywa Unahodha City

Carlos Tevez

Carlos Tevez amenyang'anywa rasmi Unahodha wa timu ya Man City na Meneja wa Timu hiyo Roberto Mancini.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentine, ambaye kwa kipindi kirefu cha usajili amekuwa akitafuta timu ya kuhamia, nafasi yake ya Unahodha amepewa mlinzi wa timu hiyo Vincent Kompany.
Mancini alisema: "Carlos alikuwa anataka kuondoka kwa sababu za kifamilia, nikaheshimu maamuzi yake, ila Carlos bado yuko hapa sababu hatukupata ufumbuzi.
"Niliamua kwenye kipindi cha majira ya joto Vinnie [Kompany] ndiye awe Nahodha wa timu."

Young: Hakuna uhakika wa namba United

Ashley Young

Licha ya kuanza vyema msimu kama mchezaji wa Manchester United, Ashley Young anasema inabidi aendelee kukaza buti ili aweze kuendelea kuwemo kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Mchezaji huyo wa kimataifa toka Uigereza amejiunga na Mashetani Wekundu kwa gharama ya £15 ml toka Klabu ya Aston Villa katika kipindi cha majira ya joto, huku akiweza kuendana haraka na mfumo wa kimchezo wa vijana wa Old Trafford.
Ameweza kufunga magoli mawili kwenye mechi ya Pemier League dhidi ya Arsenal, mechi iliyoisha kwa Man U kupata ushindi wa goli 8-2, huku akitoa pasi nne za kufunga.
Uwepo wa Ryan Giggs, Park Ji-Sung na Antonio Valencia ni ishara tosha ya ugumu wa namba kwenye nafasi yake.
"Mazingira kwenye nafasi yangu ni mazuri, najisikia kama nimepokewa kwa mikono miwili," Young alisema. "Nimeweza kuendana na mfumo wa kikosi haraka, binasfi naona ni rahisi kuendana nao."
"Kila mtu ana hali ya ushindi na anataka namba kwenye kikosi cha kwanza - inabidi kuwa makini."