Saturday, September 10, 2011

Tevez anyang'anywa Unahodha City

Carlos Tevez

Carlos Tevez amenyang'anywa rasmi Unahodha wa timu ya Man City na Meneja wa Timu hiyo Roberto Mancini.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentine, ambaye kwa kipindi kirefu cha usajili amekuwa akitafuta timu ya kuhamia, nafasi yake ya Unahodha amepewa mlinzi wa timu hiyo Vincent Kompany.
Mancini alisema: "Carlos alikuwa anataka kuondoka kwa sababu za kifamilia, nikaheshimu maamuzi yake, ila Carlos bado yuko hapa sababu hatukupata ufumbuzi.
"Niliamua kwenye kipindi cha majira ya joto Vinnie [Kompany] ndiye awe Nahodha wa timu."

No comments:

Post a Comment