Saturday, September 10, 2011

Yanga kukata kiu ya mashabiki wake leo?

Mashabiki wa Yanga
MASHABIKI wa Yanga wenye kiu ya ushindi wa takribani siku 62, watajazana kwenye Uwanja Taifa kuwaongoza mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu kusaka pointi tatu dhidi ya vibonde Ruvu Shooting leo.

Yanga wanashuka uwanjani hapo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Simba katika mechi ya fainali ya Kombe la Kagame iliyofanyika Julai 10 yakiwa ni matokeo yao mazuri ya mwisho katika mechi zaidi ya saba walizocheza tangu wacheze mechi hiyo.

Mabingwa hao walikuwa kwenye wakati mgumu kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro waliouteua kuwa uwanja wa nyumbani baada ya serikali kuufunga Uwanja wa Taifa kwa takribani wiki mbili.

Katika mchezo wa leo dhidi ya Shooting, vijana hao wa mtaa wa Twiga na Jangwani wanajua mashabiki wao wana hamu kubwa ya kuona timu hiyo ikirudisha heshima yake kwa kushinda mchezo wa kwanza katika Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment