Saturday, September 10, 2011

Young: Hakuna uhakika wa namba United

Ashley Young

Licha ya kuanza vyema msimu kama mchezaji wa Manchester United, Ashley Young anasema inabidi aendelee kukaza buti ili aweze kuendelea kuwemo kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Mchezaji huyo wa kimataifa toka Uigereza amejiunga na Mashetani Wekundu kwa gharama ya £15 ml toka Klabu ya Aston Villa katika kipindi cha majira ya joto, huku akiweza kuendana haraka na mfumo wa kimchezo wa vijana wa Old Trafford.
Ameweza kufunga magoli mawili kwenye mechi ya Pemier League dhidi ya Arsenal, mechi iliyoisha kwa Man U kupata ushindi wa goli 8-2, huku akitoa pasi nne za kufunga.
Uwepo wa Ryan Giggs, Park Ji-Sung na Antonio Valencia ni ishara tosha ya ugumu wa namba kwenye nafasi yake.
"Mazingira kwenye nafasi yangu ni mazuri, najisikia kama nimepokewa kwa mikono miwili," Young alisema. "Nimeweza kuendana na mfumo wa kikosi haraka, binasfi naona ni rahisi kuendana nao."
"Kila mtu ana hali ya ushindi na anataka namba kwenye kikosi cha kwanza - inabidi kuwa makini."

No comments:

Post a Comment