Saturday, September 10, 2011

Mrithi wa Genevive kupatikana leo

Genevive Miss Tanzania 2010
SHINDANO la kumsaka mrembo wa Miss Tanzania linafanyika leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Jumla ya warembo 30 watapanda jukwaani kuchuana vikali kuwania zawadi ya gari aina ya Jeep Patriot yenye thamani ya shilingi 72 milioni.
Warembo hao wataonyesha vazi la ubunifu, ufukweni na vazi la usiku.
Mshindi atapata fursa ya kuiwakilisha Tanzania kwenye shindano la urembo la dunia 'Miss World' litakalofanyika baadaye mwaka huu.

No comments:

Post a Comment