Sunday, September 11, 2011

Salha Israel: Miss TZ 2011


Hatimaye zoezi lililochukua miezi kadhaa la kumtafuta mrembo mpya wa Tanzania kwa mwaka huu wa 2011(Miss Tanzania 2011), lilifikia kilele chake jana usiku katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar-es-salaam na mwanadada Salha Israel kuibuka mshindi na hivyo kuvikwa rasmi taji la Miss Tanzania 2011 kutoka kwa Genevive Emmanuel Mpangala (Miss Tanzania 2010) aliyekuwa akilishikilia taji hilo mpaka hapo jana.

Katika kilele cha shindano hilo lililodhaminiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni ya Vodacom na kupambwa na burudani ya mziki kutoka kwa wasanii mbalimbali wanaotamba Afrika Mashariki na Kati kama vile Diamond,Bob Junior,Kidumu na wengineo,mshindi wa pili alikuwa Tracy Sospeter na mshindi wa tatu akawa Alexia William.

No comments:

Post a Comment