Tuesday, September 13, 2011

Upatikanaji wa Tiketi mechi za Simba na Yanga Uwanja wa Chamazi


Tiketi kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zinazohusisha timu za Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam hazitauzwa uwanjani. Lengo ni kuwaondolea usumbufu mashabiki ambao wanakwenda kwenye mechi hizo na kukuta tiketi zimekwisha, hivyo kuweza kuwa chanzo cha vurugu.

Ili kujiridhisha Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilifanya uhakiki na kubaini Uwanja wa Azam una uwezo wa kuchukua watazamaji 5,000 tu na si 7,000 kama ilivyoelezwa awali. Hata hivyo lengo la mmiliki wa uwanja huo ni kuongeza viti hadi kufikia 7,500.

Kwa mantiki hiyo tiketi zitakazouzwa kwa mechi za Yanga na Simba kwenye uwanja huo ni 5,000 tu. Vituo vya kuuzia tiketi hizo siku moja kabla ya mchezo na siku yenyewe ya mchezo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Kituo cha Mafuta cha OilCom kilichoko Ubungo na Mbagala Rangitatu.

Viingilio kwa mechi za timu hizo zitakazochezwa Uwanja wa Azam ni sh. 20,000 kwa jukwaa kuu lenye uwezo wa kuchukua watazamaji 400 wakati majukwaa ya kawaida itakuwa sh. 7,000. Ili kuhakikisha idadi ya mashabiki haizidi uwezo wa uwanja hakutakuwa na tiketi za bure (complimentary).

Hivyo kutokana na kuwepo vituo vya kuuzia tiketi katika maeneo yaliyotajwa, mashabiki ambao watakosa tiketi hawana sababu ya kwenda uwanjani. Simba na Yanga zitaanza kuutumia uwanja huo kesho (Septemba 14 mwaka huu) kwa Simba kuwa mwenyeji wa Polisi Dodoma wakati siku inayofuata Yanga itakuwa mgeni wa African Lyon.

Sendeu kwa Pilato Tibaigana



Sekretarieti ya TFF itawasilisha mashtaka dhidi ya Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi inayoongozwa na Kamishna wa Polisi mstaafu Alfred Tibaigana kutokana na matamshi yake dhidi ya mwamuzi Alex Mahagi.

Mara baada ya mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Septemba 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1, Sendeu aliita mkutano na waandishi wa habari na kumshutumu Mahagi kuwa alisababisha timu yake ikose ushindi kwa kuwabeba wapinzani wao.

Aliongeza kuwa anamfahamu Mahagi kuwa ni mwanachama wa Simba, kadi nyekundu aliyompa kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima si halali na alifanya hivyo kwa lengo la kuisadia Simba ili iendelee kukaa kileleni mwa ligi.

Kauli ya Sendeu ililenga kumjengea chuki Mahagi mbele ya mashabiki wa Yanga kama ilivyo kwa viongozi na watendaji wa TFF. Ni wazi Sendeu akiwa ofisa wa Yanga anajua taratibu za kufanya pale klabu yake isiporidhishwa na uamuzi wa mwamuzi au suala lingine lolote.

Matamshi ya Sendeu yanalenga kuchochea chuki na vurugu katika mpira wa miguu ambapo ni kinyume na Ibara ya 53(1) na (2) ya Kanuni za Nidhamu za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Kombe la Mabingwa Barani Ulaya

Usikose uhondo huu kuanzia Saa 3:45 Usiku

Bayern Munich | Villarreal | Manchester City | Napoli
Inter Milan | CSKA Moscow | Lille | Trabzonspor
Manchester United | Benfica | Basel | Otelul Galati
Real Madrid | Lyon | Ajax | Dinamo Zagreb
Chelsea| Valencia | Bayer Leverkusen | Genk
Arsenal | Marseille | Olympiakos | Borussia Dortmund
FC Porto | Shakhtar Donetsk | Zenit St Petersburg | APOEL
Barcelona | AC Milan | BATE Borisov | Viktoria Plzen

Mechi za CL

Jumatano Sept. 14
Ajax v Lyon, GpD, 21:45
Basle v SC Otelul Galati, GpC, 21:45
Benfica v Man Utd, GpC, 21:45
Dinamo Zagreb v Real Madrid, GpD, 21:45
Inter Milan v Trabzonspor, GpB, 21:45
Lille v CSKA Moscow, GpB, 21:45
Man City v Napoli, GpA, 21:45
Villarreal v Bayern Munich, GpA, 21:45

Saa 3:45 Usiku

Muda ni kwa saa za Bongo

Barca yashikwa shati saa ya kifo

 
AC Milan wameweza kupata sare ya bao 2-2 dhidi ya Barcelona, baada ya mpira wa kichwa uliopigwa na Thiago Silva kutinga wavuni, kufuatia kona iliyopigwa na mkongwe Seedorf kwenye dakika za nyongeza za mechi kuisha.
 
Alex Pato aliushangaza umati wa washabiki wa Camp Nou, baada ya kuifunga moja ya goli la kihistoria ya michuano hiyo, mchezaji huyowa kimataifa toka Brazil, lifunga goli kwenye sekunde ya 24 mara tu baada ya mpira kuanza, na kuwafanya Milan wawe mbele kwa bao moja.
 
Barca walipigana kiume, ambapo Pedro aliweza sawazisha goli kwa shuti la karibu, halafu David Villa akaongeza la pili kutokana na mpira wa adhabu.
 
Arsenal waliporwa tonge mdomoni, baada ya bao la Ivan Perisic alilolifunga dakika za majeruhi kuiwezesha Dortmund kupata sare ya goli 1-1, huku goli la Arsenal likiwekwa kimiani na Robie Van Persie.
 
Kwengineko Porto, Chelsea, Apoel Nicosia na Marseille walianza vyema michuano hiyo kwa ushindi.
 
Matokeo ya Mechi za CL
Jumanne, 13 September 2011
 
Apoel Nicosia 2-1 Zenit St Petersburg
Barcelona 2-2 AC Milan
Borussia Dortmund 1-1 Arsenal
Chelsea 2-0 Bayer Leverkusen
FC Porto 2-1 Shakhtar Donetsk
Genk 0-0 Valencia
Olympiakos 0-1 Marseille
Plzen 1-1 BATE Borisov

Ibrahimovic kukosa mechi ya Barcelona


 
Mshambuliaji wa timu ya AC Milan Zlatan Ibrahimovic, ameondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo, na hivyo atakosa kukutana na timu yake ya zamani Barcelona.
Mechi hii ya kwanza ya Michuano ya Kombe la Mabingwa Bara la Ulaya Kundi H, itachezwa leo kwenye Uwanja wa Camp Nou.
Ibrahimovic alipata maumivu kwenye mguu, wakati wa mazoezi ya timu hiyo siku ya Jumatatu, maumivu yaliyosababisha kuachwa kwenye msafara huo ulioelekea Hispania.

Kombe la Mabingwa Barani Ulaya

Usikose uhondo huu kuanzia Saa 3:45 Usiku

 
Group A
Bayern Munich | Villarreal | Manchester City | Napoli
Group B
Inter Milan | CSKA Moscow | Lille | Trabzonspor
Group C
Manchester United | Benfica | Basel | Otelul Galati
Group D
Real Madrid | Lyon | Ajax | Dinamo Zagreb
Group E
Chelsea| Valencia | Bayer Leverkusen | Genk
Group F
Arsenal | Marseille | Olympiakos | Borussia Dortmund
Group G
FC Porto | Shakhtar Donetsk | Zenit St Petersburg | APOEL
Group H
Barcelona | AC Milan | BATE Borisov | Viktoria Plzen


Mechi za LEO:

Apoel Nicosia v Zenit St Petersburg, GpG, 21:45
Barcelona v AC Milan, GpH, 21:45
Borussia Dortmund v Arsenal, GpF,21:45
Chelsea v Bayer Leverkusen, GpE, 21:45
FC Porto v Shakhtar Donetsk, GpG, 21:45
Genk v Valencia, GpE, 21:45
Olympiakos v Marseille, GpF, 21:45
Plzen v BATE Borisov, GpH, 21:45 
Muda ni kwa saa za Bongo, Saa 3:45 Usiku

Ferdinand aachwa safari ya Ureno

Beki wa Timu ya Man U Rio Ferdinand, hajasafiri na Timu hiyo nchini Ureno kwenye mechi ya Ufunguzi Kombe la Mabigwa Barani Ulaya, mchezo utakaochezwa siku ya Jumatano dhidi ya Benfica.
Hajaelewaka moja kwa moja nini hasa sababu iliyofanya kuachwa kwake, ila inaaminika ni katika kumpa mapumziko zaidi mchezaji huyo.
Toka msimu mpya uanze mechi ya juzi dhidi ya Bolton ndio ilikuwa mechi yake ya kwanza kucheza kwa dakika zote 90 za mchezo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, sambamba na Nemanja Vidic ambaye mara kwa mara huwa wanacheza nafasi ya ulinzi wa kati wa timu hiyo naye pia hatokuwepo kwenye kikosi hicho.
Jonny Evans anategemea kuungana na beki mgeni wa kikosi hicho Phil Jones kuziba mapengo hayo.