Tuesday, September 13, 2011

Ibrahimovic kukosa mechi ya Barcelona


 
Mshambuliaji wa timu ya AC Milan Zlatan Ibrahimovic, ameondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo, na hivyo atakosa kukutana na timu yake ya zamani Barcelona.
Mechi hii ya kwanza ya Michuano ya Kombe la Mabingwa Bara la Ulaya Kundi H, itachezwa leo kwenye Uwanja wa Camp Nou.
Ibrahimovic alipata maumivu kwenye mguu, wakati wa mazoezi ya timu hiyo siku ya Jumatatu, maumivu yaliyosababisha kuachwa kwenye msafara huo ulioelekea Hispania.

No comments:

Post a Comment