Tuesday, September 13, 2011

Ferdinand aachwa safari ya Ureno

Beki wa Timu ya Man U Rio Ferdinand, hajasafiri na Timu hiyo nchini Ureno kwenye mechi ya Ufunguzi Kombe la Mabigwa Barani Ulaya, mchezo utakaochezwa siku ya Jumatano dhidi ya Benfica.
Hajaelewaka moja kwa moja nini hasa sababu iliyofanya kuachwa kwake, ila inaaminika ni katika kumpa mapumziko zaidi mchezaji huyo.
Toka msimu mpya uanze mechi ya juzi dhidi ya Bolton ndio ilikuwa mechi yake ya kwanza kucheza kwa dakika zote 90 za mchezo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, sambamba na Nemanja Vidic ambaye mara kwa mara huwa wanacheza nafasi ya ulinzi wa kati wa timu hiyo naye pia hatokuwepo kwenye kikosi hicho.
Jonny Evans anategemea kuungana na beki mgeni wa kikosi hicho Phil Jones kuziba mapengo hayo.

No comments:

Post a Comment