Tuesday, September 13, 2011

Barca yashikwa shati saa ya kifo

 
AC Milan wameweza kupata sare ya bao 2-2 dhidi ya Barcelona, baada ya mpira wa kichwa uliopigwa na Thiago Silva kutinga wavuni, kufuatia kona iliyopigwa na mkongwe Seedorf kwenye dakika za nyongeza za mechi kuisha.
 
Alex Pato aliushangaza umati wa washabiki wa Camp Nou, baada ya kuifunga moja ya goli la kihistoria ya michuano hiyo, mchezaji huyowa kimataifa toka Brazil, lifunga goli kwenye sekunde ya 24 mara tu baada ya mpira kuanza, na kuwafanya Milan wawe mbele kwa bao moja.
 
Barca walipigana kiume, ambapo Pedro aliweza sawazisha goli kwa shuti la karibu, halafu David Villa akaongeza la pili kutokana na mpira wa adhabu.
 
Arsenal waliporwa tonge mdomoni, baada ya bao la Ivan Perisic alilolifunga dakika za majeruhi kuiwezesha Dortmund kupata sare ya goli 1-1, huku goli la Arsenal likiwekwa kimiani na Robie Van Persie.
 
Kwengineko Porto, Chelsea, Apoel Nicosia na Marseille walianza vyema michuano hiyo kwa ushindi.
 
Matokeo ya Mechi za CL
Jumanne, 13 September 2011
 
Apoel Nicosia 2-1 Zenit St Petersburg
Barcelona 2-2 AC Milan
Borussia Dortmund 1-1 Arsenal
Chelsea 2-0 Bayer Leverkusen
FC Porto 2-1 Shakhtar Donetsk
Genk 0-0 Valencia
Olympiakos 0-1 Marseille
Plzen 1-1 BATE Borisov

No comments:

Post a Comment