Saturday, September 10, 2011

Maradona: Sijawahi angalia mechi ya Argentina

Diego Maradona

Kocha wa timu ya Al-Wasl Diego Maradona, amesema hawezi thubutu kuangalia mechi ya Timu ya Taifa ya Argentina.
Kocha huyo ambaye hivi karibuni ameanza kutafuta mafanikio mapya Mashariki ya Kati amesema, " Toka nilipoondoka, sijawahi kuangalia hata mechi moja ya Argentina"
"Sidhani kama ntakuja kuangalia tena, najua itaniumiza" alisema nguli huyo wa zamani mwenye miaka 50 sasa.

"Sina deni na mtu, nilijitahidi kujitoa kwa yote kwa wachezaji, nao walifanya kwangu kama mimi ilivyofanya kwao."

"Hatukuweza kuwapa Wa-Argentina kile walichopaswa kukipata, ambacho kilikuwa ni Kombe la Dunia, ila tulijitahidi kadiri tulivyoweza, na tunajiangalia kwenye kioo na fahari."

No comments:

Post a Comment