Thursday, September 8, 2011

Usishangae Beckham QPL January

David Beckham

Litakapokuja kufunguliwa dirisha la usajili, usishangae Queens Park Rangers wakionyesha nia ya kumtaka David Beckham, ambaye mkataba wake kwenye Major League Soccer unaisha mwezi November.
"Ila hiyo haitakuwa mpaka mwezi January, hakika hiki si kitu cha kuzungumza kwa sasa." Haya ni maneno ya Kocha mkuu wa timu hiyo Neil Warnock.
"Hatuwezi kumsajili ila, hatuwezi kumsajili mtu yoyote kwa sasa mpaka January, kwa nini muwe na wasi?" Warnock alisema siku ya Alhamisi, wiki moja baada ya dirisha la usajili kufungwa.
"Nadhani ni mchezaji wa kipekee, na amekuwa hazina kubwa kwa soka la Uingereza, nampenda kama mtu ila niulize itapofika January.” Alisema Warnock.

No comments:

Post a Comment