Thursday, September 8, 2011

Dalglish amtetea Carroll

Andy Carroll

Meneja wa Klabu ya Liverpool Kenny Dalglish, amemtetea mchezaji wake Andy Carroll, kufuatia shutuma alizotupiwa na Kocha wa Timu ya Taifa ya Uingereza Fabio Capello, juu ya kiwango cha mchezaji huyo na tabia ya anasa inayoporomosha kiwango chake.

Mapema wiki hii, Mtalianao huyo alisema: "Andy anahitaji kuwa makini. Sijui chochote kuhusu aina hii ya maisha, ni matatizo binafsi ambayo siwezi kuyazungumzia.

"Ila kama anahitaji kuwa mchezaji mzuri na mwanamichezo, anahitaji apunguze kupunguza kunywa, hayupo kwenye kiwango chake cha juu kwa sasa."

Ila Dalglish ambaye alitumia kiasi cha £35m mwezi January alimtetea kwa kusema, "kwetu sisi tumezungumza mara kadhaa, ila imeangukia kwenye sikio la kiziwi, Andy hakuwa fiti kiasi cha kutosha msimu uliopita sababu ya majeraha,'' alisema meneja huyo.

"Tumeridhishwa na kiwango cha ufiti wake kwa mwaka huu, sababu ameondokana na majeraha yaliyokuwa yanamkabili."

"Haufahamu maisha yake, nani anafahamu maisha yake? Andy, nadhani ni mtu mwenye hekima zaidi ya watu wengi sana, na sidhani mwenendo wa maisha wake si kitu pale wanapotaka kuandika habari zao.

"Nadhani anashukuru ushauri wa Fabio Capello, na anamuheshimu sana Fabio Capello - na naamini pia Fabio Capello anamuheshimu sana Andy Carroll.''

No comments:

Post a Comment