Wednesday, September 7, 2011

Ferguson: Sneijder si wakufananishwa na Scholes

Xavi & Paul Scholes

KOCHA wa Klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson, amesema Wesley Sneijder asingeweza kuwa mtu sahihi kama mtu mbadala wa kumrithi Paul Scholes ndani ya Manchester United, huku akisisitiza ni wachezaji wa Barcelona pekee yaani Xavi na Andres Iniesta ndio umbao ungeweza kuwafananisha na mchezaji huyo na kiungo wa zamani wa Uingereza.
"Sneijder si aina ya mchezaji anayeweza kuwa mbadala wa Scholes," Ferguson alisema.

"Ni mchezaji mzuri, lakini hakuwa aina ya mchezaji tuliyekuwa tunamtafuta kuweza kumrith Scholes. Ni Xavi na Iniesta pekee ndio unaoweza kuwalinganisha na Scholes."

No comments:

Post a Comment