Wednesday, September 7, 2011

TFF yatangaza mapato ya pambano la Stars


Pambano la mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Algeria (Desert Warriors) limeingiza sh.148,220,000.

Mechi hiyo ilichezwa Septemba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mashabiki waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo ni 29,892.

No comments:

Post a Comment