Wednesday, September 7, 2011

Meireles akana Pesa kumuondoa Liverpool

Raul Meireles

Mchezaji wa kimataifa wa Ureno Raul Meireles, amesisitiza kwamba hela si kitu ambacho kilimshawishi kufanya uhamisho wa kushtukiza toka Liverpool na kuhamia Chelsea.

"Haya ni mambo yanayotokea kwenye mpira wa miguu. Nitasema vitu vizuri tu kuhusu Liverpool, nilikuwa na mwaka mmoja mzuri," Meireles aliieleza *RTPN*.

"Watu wanafikiri mimi ni Yuda na nilihama kwa sababu ya hela. Hiyo haikuwa sababu, nitaelezea wakati mwengine, kwa sasa bado ni mapema.

No comments:

Post a Comment