Thursday, September 15, 2011

Iniesta nje Mwezi Mmoja


Klabu ya Barcelona imetangaza kwenye mtandao wake kwamba, Andres Iniesta atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa mwezi mmoja.

Kiungo huyo aliumia dakika 5 kabla ya mapumziko, kwenye mechi ambayo timu yake ilitoka sare ya 2-2 na AC Milan, katika michuano ya Kombe la mabingwa Barani Ulaya siku ya Jumanne.

Iniesta atakosa mechi dhidi ya Osasuna, Valencia, Atletico Madrid, BATE Borisov na Sporting Gijon.

Mchezaji huyo anategemea kurudi tena uwanjani kwenye mechi ya michuano ya Euro 2012, ambapo timu ya Hispania itakapocheza na Czech Republic na Scotland, mnamo tarehe 7 na 11 Oktoba.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27, ameweza kucheza jumla ya mechi 6 kwa klabu msimu huu, huku akikamilisha wastani wa dakika 469 uwanjani.

Bradley aajiriwa Misri



Inaarifiwa kwamba, Kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Marekani Bob Bradley, ameajiliwa kuwa kocha wa timu ya taifa ya Misri.

Msemaji wa EFA Azmy Megahed amesema, Bradley anategemea kuwasili Cairo wikiendi hii kukamilisha mpango huo.

"Kila kitu kipo sawa. Bradley atawasili hapa siku ya Jumapili kukamilisha mkataba," Megahed alisema.

Bradley atakuwa amechukua nafasi ya kocha wa kipindi kirefu wa timu hiyo Hassan Shehata, ambaye kibarua chake kilisitishwa mnamo mwezi June, kufuatia kufanya vibaya kwa timu hiyo kwenye kampeni zake za kushiki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2012.

Timu hiyo mpaka sasa imetolewa kwenye mbio hizo.

Bradley aliiwezesha Marekani kufika kwenye mzunguko wa 16 wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010, iliyofanyika nchini Afrika ya Kusini.

Na alipigwa chini mnamo mwezi July baada ya Marekani kufungwa 4-2 na Mexico kwenye fainali ya Gold Cup, huku nafasi yake ikichukuliwa na kocha wa zamani wa Ujerumani Jurgen Klinsmann.

Bradley atakuwa na mtihani mzito kuhakikisha nchi ya Misri inapata nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia, kwa mara ya mwisho Taifa hilo kushiriki Kombe hilo ilikuwa ni mwaka 1990.

Simba na Polisi zaingiza ml16/-


Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Polisi Dodoma iliyochezwa Septemba 14 mwaka huu Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam imeingiza sh. 16,839,000.

Watazamaji waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo walikuwa 2,257 ambapo kiingilio kilikuwa sh, 7,000 kwa mzunguko na sh. 20,000 kwa VIP. Waliokata tiketi za sh. 20,000 walikuwa 80.

Baada ya kuondoa gharama za mchezo na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 2,568,661.02 kila timu ilipata sh. 3,546,671.90. Mgawo mwingine ulikwenda kwa uwanja (sh. 1,162,893.90), TFF (sh. 1,162,893.90), Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu- FDF (sh. 581,446.95), Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam- DRFA (sh. 465,157.56) na Baraza la Michezo la Taifa- BMT (sh. 116,289.39).

Kamati ya Tibaigana Sept. 24


Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itakutana tena Septemba 24 mwaka huu kwa ajili ya kusikiliza mashauri matatu dhidi ya Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage na Ofisa Habari wa klabu ya Yanga, Louis Sendeu.

Awali kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alfred Tibaigana ilikuwa ikutane Agosti 29 mwaka huu kusikiliza malalamiko ya TFF dhidi ya viongozi hao, lakini kikao kiliahirishwa kutokana na Kamati kutotimiza akidi (column) kwa wajumbe wake.

Pia TFF imewasilisha kwa kamati hiyo shauri jipya dhidi ya Sendeu kutokana na matamshi yake dhidi ya mwamuzi Alex Mahagi aliyechezesha mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Septemba 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Sendeu alimshutumu Mahagi kuwa alisababisha timu yake ikose ushindi kwa kuwabeba wapinzani wao, na anamfahamu Mahagi kuwa ni mwanachama wa Simba na kadi nyekundu aliyompa kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima haikuwa halali.

Wednesday, September 14, 2011

Fergie: Rooney ni kama Pele


Meneja wa klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson, amemfananisha mshambuliaji wa timu yake Wayne Rooney na mchezaji mkongwe wa Brazil Pele.

Fergie ameyasema hayo, kuelelekea kwenye mechi ya Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya Benfica, mechi inayotarajiwa kuchezwa usiku huu, huku mchezaji huyo akionekana kuwa kwenye kiwango kizuri kiuchezaji.

Tuesday, September 13, 2011

Upatikanaji wa Tiketi mechi za Simba na Yanga Uwanja wa Chamazi


Tiketi kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zinazohusisha timu za Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam hazitauzwa uwanjani. Lengo ni kuwaondolea usumbufu mashabiki ambao wanakwenda kwenye mechi hizo na kukuta tiketi zimekwisha, hivyo kuweza kuwa chanzo cha vurugu.

Ili kujiridhisha Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilifanya uhakiki na kubaini Uwanja wa Azam una uwezo wa kuchukua watazamaji 5,000 tu na si 7,000 kama ilivyoelezwa awali. Hata hivyo lengo la mmiliki wa uwanja huo ni kuongeza viti hadi kufikia 7,500.

Kwa mantiki hiyo tiketi zitakazouzwa kwa mechi za Yanga na Simba kwenye uwanja huo ni 5,000 tu. Vituo vya kuuzia tiketi hizo siku moja kabla ya mchezo na siku yenyewe ya mchezo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Kituo cha Mafuta cha OilCom kilichoko Ubungo na Mbagala Rangitatu.

Viingilio kwa mechi za timu hizo zitakazochezwa Uwanja wa Azam ni sh. 20,000 kwa jukwaa kuu lenye uwezo wa kuchukua watazamaji 400 wakati majukwaa ya kawaida itakuwa sh. 7,000. Ili kuhakikisha idadi ya mashabiki haizidi uwezo wa uwanja hakutakuwa na tiketi za bure (complimentary).

Hivyo kutokana na kuwepo vituo vya kuuzia tiketi katika maeneo yaliyotajwa, mashabiki ambao watakosa tiketi hawana sababu ya kwenda uwanjani. Simba na Yanga zitaanza kuutumia uwanja huo kesho (Septemba 14 mwaka huu) kwa Simba kuwa mwenyeji wa Polisi Dodoma wakati siku inayofuata Yanga itakuwa mgeni wa African Lyon.

Sendeu kwa Pilato Tibaigana



Sekretarieti ya TFF itawasilisha mashtaka dhidi ya Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu kwenye Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi inayoongozwa na Kamishna wa Polisi mstaafu Alfred Tibaigana kutokana na matamshi yake dhidi ya mwamuzi Alex Mahagi.

Mara baada ya mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Septemba 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1, Sendeu aliita mkutano na waandishi wa habari na kumshutumu Mahagi kuwa alisababisha timu yake ikose ushindi kwa kuwabeba wapinzani wao.

Aliongeza kuwa anamfahamu Mahagi kuwa ni mwanachama wa Simba, kadi nyekundu aliyompa kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima si halali na alifanya hivyo kwa lengo la kuisadia Simba ili iendelee kukaa kileleni mwa ligi.

Kauli ya Sendeu ililenga kumjengea chuki Mahagi mbele ya mashabiki wa Yanga kama ilivyo kwa viongozi na watendaji wa TFF. Ni wazi Sendeu akiwa ofisa wa Yanga anajua taratibu za kufanya pale klabu yake isiporidhishwa na uamuzi wa mwamuzi au suala lingine lolote.

Matamshi ya Sendeu yanalenga kuchochea chuki na vurugu katika mpira wa miguu ambapo ni kinyume na Ibara ya 53(1) na (2) ya Kanuni za Nidhamu za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Kombe la Mabingwa Barani Ulaya

Usikose uhondo huu kuanzia Saa 3:45 Usiku

Bayern Munich | Villarreal | Manchester City | Napoli
Inter Milan | CSKA Moscow | Lille | Trabzonspor
Manchester United | Benfica | Basel | Otelul Galati
Real Madrid | Lyon | Ajax | Dinamo Zagreb
Chelsea| Valencia | Bayer Leverkusen | Genk
Arsenal | Marseille | Olympiakos | Borussia Dortmund
FC Porto | Shakhtar Donetsk | Zenit St Petersburg | APOEL
Barcelona | AC Milan | BATE Borisov | Viktoria Plzen

Mechi za CL

Jumatano Sept. 14
Ajax v Lyon, GpD, 21:45
Basle v SC Otelul Galati, GpC, 21:45
Benfica v Man Utd, GpC, 21:45
Dinamo Zagreb v Real Madrid, GpD, 21:45
Inter Milan v Trabzonspor, GpB, 21:45
Lille v CSKA Moscow, GpB, 21:45
Man City v Napoli, GpA, 21:45
Villarreal v Bayern Munich, GpA, 21:45

Saa 3:45 Usiku

Muda ni kwa saa za Bongo

Barca yashikwa shati saa ya kifo

 
AC Milan wameweza kupata sare ya bao 2-2 dhidi ya Barcelona, baada ya mpira wa kichwa uliopigwa na Thiago Silva kutinga wavuni, kufuatia kona iliyopigwa na mkongwe Seedorf kwenye dakika za nyongeza za mechi kuisha.
 
Alex Pato aliushangaza umati wa washabiki wa Camp Nou, baada ya kuifunga moja ya goli la kihistoria ya michuano hiyo, mchezaji huyowa kimataifa toka Brazil, lifunga goli kwenye sekunde ya 24 mara tu baada ya mpira kuanza, na kuwafanya Milan wawe mbele kwa bao moja.
 
Barca walipigana kiume, ambapo Pedro aliweza sawazisha goli kwa shuti la karibu, halafu David Villa akaongeza la pili kutokana na mpira wa adhabu.
 
Arsenal waliporwa tonge mdomoni, baada ya bao la Ivan Perisic alilolifunga dakika za majeruhi kuiwezesha Dortmund kupata sare ya goli 1-1, huku goli la Arsenal likiwekwa kimiani na Robie Van Persie.
 
Kwengineko Porto, Chelsea, Apoel Nicosia na Marseille walianza vyema michuano hiyo kwa ushindi.
 
Matokeo ya Mechi za CL
Jumanne, 13 September 2011
 
Apoel Nicosia 2-1 Zenit St Petersburg
Barcelona 2-2 AC Milan
Borussia Dortmund 1-1 Arsenal
Chelsea 2-0 Bayer Leverkusen
FC Porto 2-1 Shakhtar Donetsk
Genk 0-0 Valencia
Olympiakos 0-1 Marseille
Plzen 1-1 BATE Borisov

Ibrahimovic kukosa mechi ya Barcelona


 
Mshambuliaji wa timu ya AC Milan Zlatan Ibrahimovic, ameondolewa kwenye kikosi cha timu hiyo, na hivyo atakosa kukutana na timu yake ya zamani Barcelona.
Mechi hii ya kwanza ya Michuano ya Kombe la Mabingwa Bara la Ulaya Kundi H, itachezwa leo kwenye Uwanja wa Camp Nou.
Ibrahimovic alipata maumivu kwenye mguu, wakati wa mazoezi ya timu hiyo siku ya Jumatatu, maumivu yaliyosababisha kuachwa kwenye msafara huo ulioelekea Hispania.

Kombe la Mabingwa Barani Ulaya

Usikose uhondo huu kuanzia Saa 3:45 Usiku

 
Group A
Bayern Munich | Villarreal | Manchester City | Napoli
Group B
Inter Milan | CSKA Moscow | Lille | Trabzonspor
Group C
Manchester United | Benfica | Basel | Otelul Galati
Group D
Real Madrid | Lyon | Ajax | Dinamo Zagreb
Group E
Chelsea| Valencia | Bayer Leverkusen | Genk
Group F
Arsenal | Marseille | Olympiakos | Borussia Dortmund
Group G
FC Porto | Shakhtar Donetsk | Zenit St Petersburg | APOEL
Group H
Barcelona | AC Milan | BATE Borisov | Viktoria Plzen


Mechi za LEO:

Apoel Nicosia v Zenit St Petersburg, GpG, 21:45
Barcelona v AC Milan, GpH, 21:45
Borussia Dortmund v Arsenal, GpF,21:45
Chelsea v Bayer Leverkusen, GpE, 21:45
FC Porto v Shakhtar Donetsk, GpG, 21:45
Genk v Valencia, GpE, 21:45
Olympiakos v Marseille, GpF, 21:45
Plzen v BATE Borisov, GpH, 21:45 
Muda ni kwa saa za Bongo, Saa 3:45 Usiku

Ferdinand aachwa safari ya Ureno

Beki wa Timu ya Man U Rio Ferdinand, hajasafiri na Timu hiyo nchini Ureno kwenye mechi ya Ufunguzi Kombe la Mabigwa Barani Ulaya, mchezo utakaochezwa siku ya Jumatano dhidi ya Benfica.
Hajaelewaka moja kwa moja nini hasa sababu iliyofanya kuachwa kwake, ila inaaminika ni katika kumpa mapumziko zaidi mchezaji huyo.
Toka msimu mpya uanze mechi ya juzi dhidi ya Bolton ndio ilikuwa mechi yake ya kwanza kucheza kwa dakika zote 90 za mchezo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, sambamba na Nemanja Vidic ambaye mara kwa mara huwa wanacheza nafasi ya ulinzi wa kati wa timu hiyo naye pia hatokuwepo kwenye kikosi hicho.
Jonny Evans anategemea kuungana na beki mgeni wa kikosi hicho Phil Jones kuziba mapengo hayo.

Monday, September 12, 2011

Aguero: Ajipanga kuwa Maradona wa City


Sergio Aguero anaonekana kuwa mchezaji muhimu ndani ya Manchester City, umuhimu kama aliokuwa nao Diego Maradona wakati alipokuwa anaichezea Napoli.

Aguero, ambaye amemuoa mtoto wa Maradona, amefunga magoli sita kwenye mechi nne alizoichezea City, toka ajiunge nayo kwa dau la £38 ml alipotokea timu ya Atletico Madrid, kwenye kipindi cha majira ya joto.

Na anapewa nafasi kubwa ya kuiongoza na kuiwezesha City kwenye ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza, kama ambavyo Maradona alifanya akiwa na Napoli.

Maradona aliiwezesha timu hiyo ya Italia kushinda Serie A mara mbili, Kombe la UEFA na Coppa Italia, wakati mchezaji huyo toka Argentina alipokuwa kwenye hiyo timu.

"Naamini ntaweza kuisaidia Manchester City kufanya mambo makubwa kama Diego alivyofanya akiwa na Napoli," Aguero alisema.

"Nimekuja hapa kuisaidia timu kukua na iweze kushinda makombe, na kama tukifanya hivyo mwaka huu itakuwa ni vizuri sana,. Ila tutajitahidi kuwa wazuri zaidi na nategemea kutoa mchango mkubwa  kwenye hilo."

Evra: Lazma tuwe makini

  
Patrice Evra amewaasa wachezaji wenzake wa Manchester United, kuwa makini na kuendelea kukaza buti baada ya kuanza msimu mpya wa ligi kwa rekodi nzuri.

"Tunafanya na inaonekana kama rahisi, lakini si kweli." Alisema alipokuwa anaongea na gazeti la The Independent, "Ninawaheshimu sana Manchester City - wana kikosi makini sana."

"Walipoifunga Tottenham 5-1, tuliiangalia mechi na tukasema ni vyema tukacheza vizuri tukikutana na Arsenal - na tukafanikiwa kushinda kwa goli nane."

"Inaonekana kama ni mashindano kati ya timu hizi mbili, ila msisahaua Chelsea na Liverpool. Japokuwa, kila niwaonapo watu kitu cha kwanza kwao kuuliza ni tarehe ya mechi na wapinzani wetu."

Viingilio Mechi za Chamazi

Timu za Simba na Yanga zitaanza kuutumia Uwanja wa Azam Chamazi ulioko Mbande, Dar es Salaam wiki hii. Septemba 14 mwaka huu Simba itakuwa mwenyeji wa Polisi Dodoma wakati siku inayofuata African Lyon itakuwa mwenyeji wa Yanga.

Kwa mujibu wa msemaji wa Shirikisho hili Boniface Wambura, Viingilio kwa mechi zinazohusisha timu za Yanga na Simba kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua mashabiki 7,000 tu vitakuwa sh. 15,000 kwa jukwaa kuu na sh. 5,000 mzunguko.

Kwa timu nyingine za Dar es Salaam zinazotumia uwanja huo kiingilio kitaendelea kuwa kile kile cha sh. 10,000 jukwaa kuu na sh. 3,000 mzunguko.

Simba na Azam zaingiza Ml. 72


Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Azam na Simba iliyochezwa Septemba 11 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 72,167,000.

Kwa mujibu wa msemaji wa Shirikisho hili Boniface Wambura, Watazamaji waliokata tiketi kwa ajili ya kushuhudia mechi hiyo walikuwa 21,129. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 15,000, sh. 7,000, sh. 5,000 na sh. 3,000.

Viti vya bluu na kijani ambavyo kiingilio kilikuwa sh. 3,000 viliingiza watazamaji 18,586, hivyo kuingiza sh. 55,758,000.

Marekebisho Mechi za Uwanja wa Taifa

Ili kutekeleza maagizo ya Serikali kucheza mechi mbili tu za Ligi Kuu ya Vodacom kwenye Uwanja wa Taifa, Shirikisho la Soka Nchini (TFF) limefanya marekebisho kwa baadhi ya mechi zilizokuwa zichezwe kwenye uwanja huo.

Kwa mujibu wa msemaji wa Shirikisho hili Boniface Wambura sasa, mechi zitakazochezwa Uwanja wa Taifa ni – mechi namba 39- Azam vs Yanga (Septemba 18), mechi namba 50- Simba vs Mtibwa Sugar (Septemba 25), mechi namba 52- Yanga vs Coastal Union (Septemba 28) na mechi namba 58- Yanga vs Kagera Sugar (Oktoba 13).

Nyingine ni mechi namba 62- Simba vs African Lyon (Oktoba 16), mechi namba 65- Yanga vs Toto Africans (Oktoba 20), mechi namba 72- Simba vs JKT Ruvu (Oktoba 22), mechi namba 78- Yanga vs Simba (Oktoba 29) na mechi namba 86- Moro United vs Simba (Novemba 2).

Mechi zifuatazo zitachezwa Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam; mechi namba 35- Simba vs Polisi Dodoma (Septemba 14), mechi namba 29- African Lyon v Yanga (Septemba 15), mechi namba 45- Yanga vs Villa Squad (Septemba 21), mechi namba 66- Simba vs Ruvu Shooting (Oktoba 19) na mechi namba 71- Yanga vs Oljoro JKT (Oktoba 23).

Mapato Mechi ya Yanga na Ruvu Shooting


Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Septemba 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 23,388,000.

Kwa mujubu wa taarifa iliyotumwa kwa Yyombo vya Habari na Ofisa Habari na Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Boniface Wambura, inasema  Watazamaji waliokata tiketi kwa ajili ya kushuhudia mechi hiyo walikuwa 6,566. Viingilio vilikuwa sh. 15,000, sh. 7,000, sh. 5,000 na sh. 3,000.

Sunday, September 11, 2011

Salha Israel: Miss TZ 2011


Hatimaye zoezi lililochukua miezi kadhaa la kumtafuta mrembo mpya wa Tanzania kwa mwaka huu wa 2011(Miss Tanzania 2011), lilifikia kilele chake jana usiku katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar-es-salaam na mwanadada Salha Israel kuibuka mshindi na hivyo kuvikwa rasmi taji la Miss Tanzania 2011 kutoka kwa Genevive Emmanuel Mpangala (Miss Tanzania 2010) aliyekuwa akilishikilia taji hilo mpaka hapo jana.

Katika kilele cha shindano hilo lililodhaminiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni ya Vodacom na kupambwa na burudani ya mziki kutoka kwa wasanii mbalimbali wanaotamba Afrika Mashariki na Kati kama vile Diamond,Bob Junior,Kidumu na wengineo,mshindi wa pili alikuwa Tracy Sospeter na mshindi wa tatu akawa Alexia William.

Saturday, September 10, 2011

Mrithi wa Genevive kupatikana leo

Genevive Miss Tanzania 2010
SHINDANO la kumsaka mrembo wa Miss Tanzania linafanyika leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Jumla ya warembo 30 watapanda jukwaani kuchuana vikali kuwania zawadi ya gari aina ya Jeep Patriot yenye thamani ya shilingi 72 milioni.
Warembo hao wataonyesha vazi la ubunifu, ufukweni na vazi la usiku.
Mshindi atapata fursa ya kuiwakilisha Tanzania kwenye shindano la urembo la dunia 'Miss World' litakalofanyika baadaye mwaka huu.